Sunday, 8 March 2015

Simba Noma, Yaibuka Kidedea, yaichapa Yanga 1-0



Timu ya Simba SC ya jijini Dar es Salaam, leo imeendeleza ubabe dhidi ya Yanga SC baada ya kuifunga goli 1-0 goli lililowekwa kimiani na mshambuliaji Emmanuel Okwi katika dakika ya 53 kipindi cha pili.Hali hiyo imesababisha baadhi ya mashabiki wa yanga waliko AMUCTA Tabora kufunga simu zao.
Mechi hiyo ya ligi kuu imefanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ikuhudhuriwa na maelfu ya mashabiki kutoka katika pande zote za timu hizo waliofurika kwa wingi uwanjani hapo.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi Martin Saanya wa Morogoro akisaidiwa na Souda Lila wa Dar pamoja na Florent Zablon wa Dodoma ulimalizika kwa kiongo wa Yanga Haruna Niyonzima kuzawadiwa kadi nyekundu baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano.
By Kimena Nuhu